Jumanne, 6 Juni 2017
Ronaldo kataja sababu za kubadili style ya nywele zake
Kama wewe ni moja kati ya mashabiki wa soka hususani mashabiki wa soka la Ulaya na wanaompenda staa wa soka wa Real Madrid na timu ya taifa ya Ureno Cristiano Ronaldo najua utakuwa ni mmoja kati ya watu waliyomuona na muonekano tofauti kichwani.
Ronaldo ambaye amezoeleka kuwa na tabia ya kupenda kuzitunza nywele zake kiasi cha kufikia kusemwa katika mitandao ya kijamii kuwa anapenda kuziangalia nywele zake sana katika kioo akiwa anaingia uwanjani, alionekana kanyoa siku moja baada ya ushindi wa Champions League.
Leo June 6 2017 mtandao wa bleacher report umemnukuu staa huyo akitaja sababu za kunyoa nywele hizo baada ya ushindi wa 4-1 akiwa kafunga magoli mawili na kuisaidia timu yake ya Real Madrid kutwaa taji la 12 la UEFA Champions League msimu wa 2016/2017.
About the Author
Ukurasa wetu
Author & Editor
Has laoreet percipitur ad. Vide interesset in mei, no his legimus verterem. Et nostrum imperdiet appellantur usu, mnesarchum referrentur id vim.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Chapisha Maoni