Jumatano, 12 Novemba 2014

Naibu Katibu Mkuu akutana kwa mazungumzo na Mjumbe Maalum wa Marekani Eneo la Maziwa Makuu

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Rajabu Gamaha akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushiriano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb) na Mjumbe Maalum wa Marekani kwenye Ukanda wa Maziwa Makuu, Bw. Russel D. Feingold alipofika Wizarani kwa ajili ya mazungumzo. Katika mazungumzo yao waligusia mchango wa Tanzania katika suala la amani Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. 

 
Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Joseph Sokoine akiwa na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda, Bw. Innocent Shiyo wakifuatilia mazungumzo kati ya Naibu Katibu Mkuu na Bw. Russel (hawapo pichani).
Sehemu ya ujumbe uliofutatana na Bw. Russel wakifuatailia mazungumzo.
Maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakati wa mazungumzo kati ya Balozi Gamaha na Bw. Russel (hawapo pichani) Picha na Reuben Mchome

About the Author

Ukurasa wetu

Author & Editor

Has laoreet percipitur ad. Vide interesset in mei, no his legimus verterem. Et nostrum imperdiet appellantur usu, mnesarchum referrentur id vim.

Chapisha Maoni

 
Ukurasa wetu © 2015 - Mark Mugan| Designed and Developed by Mark Mugan | call +255 673 111 069