Jumatano, 13 Aprili 2016

Mhe. Rais apokea Hati za Utambulisho za Mabalozi wa Brazil, Czech na Sudan Kusini nchini

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi mpya wa Brazil nchini, Mhe. Carlos Alfonso Iglesias Puente. Hafla hiyo fupi ilifanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 13 Aprili, 2016.
Mhe. Rais akimtambulisha  kwa Balozi Puente Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga
Balozi mpya wa Brazil, Mhe. Puente akisalimiana na Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Joseph Sokoine mara baada ya kuwasilisha hati zake za utambulisho kwa Mhe. Rais.
Mhe. Balozi Puente akisalimiana na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Bi. Mindi Kasiga
Mhe. Balozi Puente akisalimiana na Afisa Mambo ya Nje, Bw. Anthony Mtafya.
Mhe. Rais akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Puente, Waziri Mahiga, Balozi Sokoine, Msaidizi wa Rais masuala ya Diplomasia, Balozi Zuhura Bundala (kulia) na Afisa kutoka Ubalozi wa Brazil (kushoto)
Mhe. Rais Magufuli akiwa kwenye mazungumzo na Balozi Puente
Balozi Puente (katikati) akipokea heshima ya wimbo wa Taifa lake mara baada ya kuwasilisha Hati za Utambulisho. Kulia ni Kaimu Mkuu wa Itifaki, Bw. James Bwana.

.......Hati za Utambulisho za Balozi wa Jamhuri ya Czech

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi mpya wa Jamhuri ya Czech mwenye makazi yake Nairobi, Kenya, Mhe. Pavel Rezac. Hafla hiyo ilifanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tareje 13 Aprili, 2016.
Mhe. Rais Magufuli akimtambulisha kwa Balozi Rezac Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga.
Waziri Mahiga akimtambulisha kwa Balozi Rezac Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Joseph Sokoine.
Balozi Rezac akisalimiana na  Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Bi. Mindi Kasiga
Mhe. Rais Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Rezac
Mhe. Rais Magufuli akiwa katika mazungumzo na Balozi Rezac
Waziri Mahiga ( wa kwanza kushoto) pamoja na Wajumbe kutoka Ikulu na Wizara ya Mambo ya Nje wakifuatilia mazungumzo kati ya Mhe. Rais Magufuli na Balozi Rezac (hawapo pichani).
Balozi Rezac akiagana na Kiongozi wa Bendi ya Polisi mara baada ya kuwasilisha Hati zake za utambulisho kwa Rais

...........Hati za Utambulisho za Balozi wa Sudan Kusini

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi mpya wa Sudan Kusini, Mhe. Mariano Deng Ngor. Hafla hiyo ilifanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tareje 13 Aprili, 2016.
Mhe. Rais Magufuli akimtambulisha kwa Balozi Ngor Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga.
Waziri Mahiga akimtambulisha kwa Balozi Ngor Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Samwel Shelukindo.
Balozi Ngor akisalimiana na  Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Bi. Mindi Kasiga
Picha ya pamoja
Mhe. Rais Magufuli akizungumza na Balozi wa Sudan Kusini nchini, Mhe. Ngor.
Balozi Ngor akisikiliza wimbo wa taifa lake mara baada ya kuwasili Ikulu kwa ajili ya kuwasilisha Hati za Utambulisho kwa Mhe. Rais. Kulia ni Kaimu Mkuu wa Itifaki, Bw. James Bwana.
Mhe. Balozi Ngor akisaini kitabu cha wageni  mara baada ya kuwasili Ikulu kwa ajili ya kuwasilisha Hati za Utambulisho kwa Mhe. Rais.
Picha na Reginald Philip

About the Author

Ukurasa wetu

Author & Editor

Has laoreet percipitur ad. Vide interesset in mei, no his legimus verterem. Et nostrum imperdiet appellantur usu, mnesarchum referrentur id vim.

Chapisha Maoni

 
Ukurasa wetu © 2015 - Mark Mugan| Designed and Developed by Mark Mugan | call +255 673 111 069